YANGA SC YATOKA SARE 0-0 DHIDI YA MAMELODI SUNDOWNS

 



NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imeshindwa kutamba kwenye uwanja wake wa nyumbani mara baada ya kulazimishwa sare na Mamelodi Sundowns 0-0.
Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam, Mamelodi waliweza kuutawala mchezo katika kipindi cha kwanza ambapo walitawala kwa asilimia 73% kwa 23% licha ya Yanga Sc kuwa na mashuti matatu yaliyolenga lango huku Mamelodi wakiwa wamepiga moja tu.

Kipindi cha pili Yanga walibadilika na kuonesha hali ya kulitaka bao la kuongoza bila mafanikio licha ya kupata nafasi za wazi nyingi.

Sifa za kipekee zimuendee mlinda mlango wa kimataifa wa Afrika Kusini, Ronwel Williams ambaye aliokoa hatari nyingi ambazo zilitengenezwa na Yanga Sc.
 
 
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA