BREAKINGS; MJAMZITO AFARIKI KISA UZEMBE WA WAUGUZI

 


Watumishi watano wa Kituo cha Afya Mikanjuni wamesimamishwa kazi kufuatia kifo cha mjamzito Fatuma Mussa Suleiman (36) mkazi wa Magaoni Jijini Tanga aliyefika kituoni hapo kwa ajili ya kujifungua na inadaiwa kuwa wahudumu wa zamu walifanya uzembe kwa kumuwekea damu ambayo hakustahili wala hakuwa na uhitaji nayo


Akitoa taarifa ya Serikali, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. James Kaji amesema baada ya kutokea uzembe kwa marehemu kuwekewa damu ambayo hakuwa na uhitaji nayo alipata uzio mkali (Allergic Reaction) na kisha kupelekea kifo chake.


"Mgonjwa alifanyiwa upasuaji ambapo alifanikiwa kupata mtoto wa kike na hakukuwa na changamoto yoyote kwa mama wala kwa mtoto baada ya upasuaji na aliendelea na matibabu chini ya uangalizi wa madaktari na wauguzi wa zamu."


"Katika wodi hiyo alipolazwa kulikuwa na mgonjwa ambaye alikuwa na uhitaji wa kuwekewa damu na ilikuwa tayari imeandaliwa, kwahiyo muuguzi aliyekuwa zamu alimwekea damu marehemu baada ya mgonjwa aliyekuwa anatakiwa kuwekewa damu" amesema DC James Kaji


Aidha, amewataja watumishi waliosimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi wa tukio hilo ni pamoja na wauguzi watatu ambao ni Fadhila Ally Hoza, Restituta Kasendo Deusdedit, pamoja na Muya Ally Mhando ambapo kwa upande wa madaktari ni Hamis Mohamed Msami pamoja na Andrew Eliasikia Kidee.



Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA