RAIS WA AWAMU YA PILI ALI HASSAN MWINYI AFARIKI DUNIA

 


Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ally Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februri 29,2024 saa 11 jioni katika Hospitali Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu kwa ya ugonjwa wa Saratani ya Mapafu. 
Ali Hassan Mwinyi aliyeongoza Serikali ya Awamu ya Pili aliingia madarakani rasmi tarehe 5 Novemba 1985. 

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza msiba huo leo ambapo amesema Mzee Mwinyi alikuwa akipatiwa matibabu tangu Novemba 2023 London Uingereza na baadaye kurejea Nchini na kuendelea na matibabu Mzena Hospital. 

Rais Samia ametangaza siku saba za maombolezo kuanzia kesho kufuatia kifo hicho.

“Kwa majonzi makubwa nasikitika kutangaza kifo cha Rais mstaafu wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi, aliyefariki dunia leo Februari 29 saa 11 jioni katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya saratani ya mapafu.

Mzee Ali Hassan Mwinyi, amekuwa akipatiwa matibabu tangu Novemba mwaka jana huko London, Uingereza na baadaye kurejea nchini na kuendelea na matibabu katika Hospitali ya Mzena,” amesema Rais Samia.

Mkuu huyo wa nchi amesema, kutokana na kifo hicho, bendera zitapepea nusu mlingoti kwa siku saba kuanzia kesho Ijumaa, Machi 1, 2024.

Mzee Mwinyi amefariki dunia akiwa na miaka 98 na miezi tisa na siku 21. Sawa na siku 36,091.


Mei 8, 1925, ndiyo tarehe ambayo Mwinyi alizaliwa. Kijiji cha Kivure, Wilaya ya Mkuranga, Pwani.

Mwinyi akiwa mtoto, alipelekwa Zanzibar kusoma madrasa (elimu ya dini ya Kiislam). Tangu hapo, Mwinyi alikulia na kusoma Zanzibar hadi kufikia daraja kubwa la uongozi.


Mwaka 1933, Mwinyi akiwa na umri wa miaka minane, aliandikishwa kuanza masomo, Shule ya Msingi Mangapwani, Unguja, Zanzibar. Alisoma hapo darasa la kwanza mpaka la nne, alilohitimu mwaka 1936. Alipomaliza darasa la nne, Mwinyi alijiunga na Shule ya kati (middle school), katika Shule ya Dole. Alisoma darasa la tano mpaka la nane mwaka 1942.


Mwaka 1943, Mwinyi alijiunga na Chuo cha Ualimu Zanzibar, aliposoma ngazi ya cheti. Alitunukiwa astashahada ya ualimu mwaka 1944. Mwinyi alijiendeleza zaidi kwenye fani ya ualimu kwa kusoma Astashahada Kuu ya Ualimu (General Certificate in Education ‘GCE’), kisha Stashahada ya ualimu, kupitia Chuo Kikuu cha Durban, Uingereza.
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA