TCRA CCC YAKUTANA NA WATOA HUDUMA ZA MAWASILIANO KUBORESHA HUDUMA KWA MTUMIAJI WA MAWASILIANO


Katika kutekeleza majukumu yake ya Kisheria Baraza la washauri la watumiaji huduma za mawasiliano (TCRA CCC), 
chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Hawa Ng'humbi
 imefanya mkutano na Umoja wa Watoa Huduma za Mawasiliano (TAMNOA) kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayomhusu mtumiaji wa huduma za mawasiliano ili kuboresha huduma kwa mtumiaji. 

Mkutano huo uliofanyika leo Jumatatu Novemba 27, 2023 pamoja na mambo mengine umeangazia changamoto za watumiaji na namna ambavyo TCRA CCC, Watoa Huduma na wadau wengine wanaweza kuzishughulikia ili kuondoa kero kwa watumiaji.

#HudumaBoraZaMawasilianoNiHakiYako
#TanzaniaYaKidijitali
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA