"Nchi nyingi zinamtamani Magufuli" Dkt. Abbas


Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbas amefunguka na kusema Balozi wa China nchini Tanzania anayemaliza muda wake Lu Youqing amedai nchi nyingi duniani zinatamani kuwa na Rais kama alivyo Dkt. John Pombe Magufuli kwa jinsi anavyoongoza nchi.

Dkt. Hassan Abbas amesema hayo kupitia mtandao wake wa twitter na kusema balozi huyo amesema siyo nchi za Afrika tu zinazotamani kupata kiongozi kama Magufuli bali ni dunia nzima inapenda kuwa na mtu kama Rais Magufuli. 
"Balozi wa China anayemaliza muda wake Dkt Lu aguswa na vita ya kimageuzi ya Rais Magufuli. Asema atamkumbuka kama mmoja wa mashujaa Afrika amesisitiza kuwa si Afrika tu bali hata duniani, nchi nyingi zinatamani kuwa na Rais kama Dkt. John Pombe Magufuli amedai Serikali ya Tanzania tangu Nyerere mpaka Rais Magufuli inasifika duniani kwa mageuzi makubwa" alisema Dkt.Hassan Abbas
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA